WAZIRI wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk. Mwigulu Lameck Nchemba, amegundulika kuwa na mgongano wa kimaslahi, kufuatia taarifa kuwa mke wake wa ndoa, ni mmoja wa wamiliki wa kampuni ya michezo ya kubahatisha. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali serikalini zinasema, mke wa Dk. Mwigulu, anayefahamika kwa jina la Neema Wilfred Ngure au Neema Mwigulu Nchemba, ni mmoja wa wamiliki wa kampuni ya Extrabet Limited.
Fadhili Emmanuel Nkurlu, aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya ambaye ni mmoja wa wanahisa wa kampuni ya mke wa Mwigulu, amethibitisha kuwa Neema ni mkurugenzi mwaanzilishi wa kampuni hiyo, iliyosajiliwa tarehe 1 Desemba 2020.
Wakati Neema anaanzisha kampuni hiyo, Mwigulu alikuwa waziri wa Katiba na Sheria. Nyaraka kutoka Wakala wa Serikali wa Leseni na Biashara (BRELA), zinaonyesha kuwa Neema anamiliki asilimia 77 ya hisa kwenye kampuni hiyo ya michezo ya kamari.
Undani wa habari hii ikiwemo mahojiano na Nkurlu, soma Gazeti la Raia Mwema, toleo la leo Ijumaa tarehe 23 Julai 2021.
Mawaziri wa aina hii hawafai Tanzania!
Kampaka Mama Samia mafuta kwa mgongo wa chupa kwa ile historia ya refa. Mama, mpe kadi nyekundu sasa.
Ile ya njano ni pale Wizara ya Fedha walichota fedha…hakuwahi kuwataja.
Zama zile alikuwa hatoi rambirambi za maafa yahusuyo Wizara yake. Imekuwa kawaida yake kusema tofauti namatendo yake. Asipowajibishwa kwa hili, Tanzania inaelekea wapi?