Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Burudika Waziri Mwakyembe akemea ‘mshiko’ kwa watangazaji
Burudika

Waziri Mwakyembe akemea ‘mshiko’ kwa watangazaji

Harrison Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Spread the love

WAZIRI wa Habari, Utamaduni na Michezo,  Harrison Mwakyembe amekemea tabia ya baadhi ya waandishi wa habari kuchukua pesa (mshiko), ili wapige redioni nyimbo za wasanii, anaandika Hamis Mguta.
Amesema hatakubali tabia hiyo iendelee na kwamba vyombo vya habari vinatakiwa kulipa pesa ili vipige nyimbo za wasanii redioni na kuzionesha katika Luninga.

Mwakyembe ameyasema hayo leo katika ukumbi wa Vijana uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na Chama cha Wasanii wa Muziki wa Dansi Nchini (CHAMUDATA).

“Ni upendeleo tu, baadhi ya wasanii ndiyo wanasikika wengine wanazimwa kabisa haiwezekani kabisa wasanii wenyewe wanakufa wakiwa maskini na majina makubwa harafu kuna wengine wanabadilisha magari kila wiki,” amesema. 

Aidha amesema kuwa atahakikisha wasanii wananufaika na kazi zao na amewataka kuwa na mshikamano katika kupigania haki katika sanaa ya muziki ikiwemo kuwa na mikataba kati ya mmiliki wa bendi.

“Nimeelezwa kuwa kuna watu wengine hawataki mikataba, hapana ni lazima walazimishwe, twende kwenye ngazi tofauti kabisa ya mahusiano kwa sababu bila maandishi tunapoteza vitu vingi sana,” amesema.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Hassan Msumali amesema kutonufaika kwa kazi zao ni changamoto kubwa zinazowakumba huku wakiomba kupewa muda wa ziada kutokana na ukomo wa muda wa saa sita usiku waliowekewa.

“Upigaji wa nyimbo za dansi katika vyombo mbalimbali vya habari hautendi haki kwa mziki wa  dansi,” amesema.

Doreen Sinare, OAfisa Mtendaji Mkuu COSOTA amesema elimu inahitajika kwa wasanii kwa kuwa wengi wao hawajui utofauti kati ya hatimiliki na hakishiriki na kuwa changamoto kubwa katika muziki wa dansi zinatokana na kutokuwa na mikataba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BurudikaMichezo

Kizz Daniel aunguruma na EP mpya ‘Thankz alot’

Spread the loveMKALI wa muziki nchini Nigeria, Kizz Daniel ametoa EP yake...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Burudika

Piga makofi kwa Mr. Eazi …achomoka na ‘The Evil Genius’

Spread the loveMAKOFI kwa Mr Eazi! Staa wa Afropop, Mr Eazi ameachia...

Burudika

Kishindo cha Afro B katika “Wo wo wo” akiwa na Rich the Kid&Rimzee

Spread the loveSTAA ambaye alitambulishwa na ngoma maarufu, Afrowave ‘Drogba’, Afro B,...

error: Content is protected !!