Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu: Ninasikitika kuacha kazi nzuri zaidi duniani
KimataifaTangulizi

Waziri Mkuu: Ninasikitika kuacha kazi nzuri zaidi duniani

Spread the love

 

“Ninasikitika kuacha kazi nzuri zaidi duniani lakini ndiyo hali halisi”, hayo ni maneno ya Waziri Mkuu wa Uingerea, Boris Johnson ambaye leo tarehe 7 Julai, 2022 ametangaza kujiuzulu wadhifa huo na sasa mchakato wa kumpata mrithi wake utaanza mapema wiki ijayo.

Akihutubia umma mbele ya vyombo vya habari, Kiongozi huyo amesema “Ninataka mjue jinsi ninavyohuzunishwa na kuacha kazi bora zaidi duniani.

“Nimekubaliana na Sir Graham Brady, mwenyekiti wa wabunge wetu wa viti maalum, kwamba mchakato wa kumchagua kiongozi mpya uanze sasa na ratiba itatangazwa wiki ijayo,” amesema na kuongea kuwa leo ameteua Baraza la Mawaziri kuhudumu huku yeye pia akiendelea kuongoza hadi kiongozi mpya atakapochaguliwa.’

“Inatia uchungu kutoona miradi yangu ikikamilika bila usimamii wangu, hata hivyo, ni jambo la kipuuzi kubadilisha serikali – na kukataa wazo la uchaguzi mkuu katika hali kama hii,” amesema.

Aidha, Johnson ambaye amehudumu katika nafasi hiyo kwa miaka mitatu, ameshukuru umma kwa upendo mkubwa waliomuonesha.

“Zaidi ya yote, ninataka kuwashukuru ninyi, umma wa Uingereza, kwa upendeleo makubwa mliyonipa,’’ amesema.

Amesema umma utahudumiwa kuanzia sasa hadi waziri mkuu mpya atakapochukua wadhifa huo.

Waziri mkuu amemaliza hotuba yake kwa kusema kwamba hadi pale atakapopatikana mbadala wake, maslahi ya umma yatatekelezwa.

“Kuwa waziri mkuu ni elimu ya kipekee – nimesafiri kila sehemu ya Uingereza na nimekutana na watu wengi wenye asili ya Uingereza ambao pia wako tayari kushughulikia matatizo ya zamani kwa njia mpya.

“Hata kama mambo yanaweza wakati mwingine kuonekana kuwa na giza nene, mustakabali wetu kwa pamoja ni jambo muhimu zaidi,’’ Johnson amesema huku akipigiwa makofi anapoondoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!