Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu mstaafu Mali afariki kizuizini
Kimataifa

Waziri Mkuu mstaafu Mali afariki kizuizini

Spread the love

WAZIRI MKUU mstaafu wa Mali, Soumeylou Boubèye Maïga amefariki dunia jana tarehe 21 Machi, 2022 katika hospitali moja iliyopo jijini Bamako.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Serikali ya kijeshi iliyochukua madarakani nchini humo, ilitoa salamu za pole kwa familia ya kiongozi huyo. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa karibu wa familia hiyo amelieleza Shirika la Habari la Reuters kuwa hali yake kiafya ilianza kuzorota kutokana na mazingira ya kuzuiliwa kwake.

Kiongozi huyo alilazwa hospitalini takriban miezi mitatu iliyopita, lakini daktari wake kushauri apelekwe nje ya nchi kwa matibabu, serikali iliyopo madarakani haikuruhusu.

Waziri Mkuu huyo alikamatwa na kisha kuwekwa chini ya waranti ya kukamatwa Agosti mwaka jana, kama sehemu ya uchunguzi wa tuhuma za rushwa katika ununuzi wa ndege ya Rais wa nchi hiyo, Ibrahim Keita ambaye litimuliwa madarakani na jeshi mapema mwaka huu.

Aidha, Maiga ambaye awali alikuwa waziri, aliteuliwa kushika nafasi ya waziri mkuu mwaka 2017 kisha akajiuzulu baada ya miaka miwili kutokana mauaji ya watu 160 kutoka kabila linalofahamika kwa jina la Fulani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!