Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri mkuu akubali yaishe, kujiuzulu leo
KimataifaTangulizi

Waziri mkuu akubali yaishe, kujiuzulu leo

Boris Johnson
Spread the love

 

WAZIIRI Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson anatarajiwa kujiuzulu kama kiongozi wa chama tawala cha Conservative baadaye leo, lakini ataendelea kuhudumu kama waziri hadi Oktoba mwaka huu.

Hatua hiyo imekuja baada ya wabunge 50 kujiuzulu kuendelea kuhudumia Serikali anayoiongoza katika kipindi cha saa 48 zilizopita. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Shirika la habari Uingereza -BBC Kiongozi mpya wa chama cha Conservative anatarajiwa kuchaguliwa na kuanza kuhudumu kama waziri mkuu kufikia mwisho wa mwezi Oktoba.

Hatua hii inajiri siku moja baada ya Johnson kusisitiza kuwa hatajiuzulu kutokana na tuhuma ambazo zimekuwa zikimuandama.

Johnson alikuwa amewaeleza wabunge kwamba ataendelea kutekeleza majukumu yake, licha ya shinikizo la kumtaka ajiuzulu, kufutia kuongezeka kwa idadi ya mawaziri wanaojiuzulu na maofisa wengine wa serikali wanaomtuhumu Johnson kwa kutochuku hatua dhidi ya maofisa wa serikali yake wanaotuhumiwa kuhusika katika unyanyasaji wa kingono

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

error: Content is protected !!