Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Waziri Makamba: Bei ya umeme Tanzania haijapanda
HabariTangulizi

Waziri Makamba: Bei ya umeme Tanzania haijapanda

Spread the love

 

WAZIRI wa Nishati nchini Tanzania, January Makamba amesema, Serikali haijapandisha bei ya umeme huku akiagiza mamlaka kuwachukulia hatua wale wote wanaoneza uvumi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Makamba amesema hayo leo Ijumaa, tarehe 10 Juni 2022, wakati akijibu swali la Mbunge wa Nyasa (CCM), Mhandisi Stella Manyanya aliyetaka kujua ukweli wa taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusu kupanda kwa bei ya umeme.

Akijibu swali hilo, Waziri Makamba amesema, “si kweli kabisa kwamba bei ya umeme imepanda na serikali inasikitishwa na wale wanaoeneza maneno na uvumi huo na tumeomba mamlaka zichukue hatua kwa hao wanaoeneza hayo.”

Waziri huyo amesema, suala la kupandisha linaanza kwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kupendekeza bei mpya kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kisha wananchi nao hushirikishwa.

“Kupandisha bei ni mchakato mrefu, unahusisha maombi ya Tanesco kwa Ewura na pia ni lazima wananchi wahusishwe na kushirikishwa na mchakato huo hauwezi kufanyika kwa siri.”

“Hivyo kuwa bei ya umeme imepandishwa si kweli na naomba taarifa hizo zipuuzwe na hatua zitachukuliwa kwa wahusika,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!