Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Majaliwa aonya watengeneza migogoro serikalini 
Habari za Siasa

Waziri Majaliwa aonya watengeneza migogoro serikalini 

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amewataka watu wanaotengeneza migogoro dhidi ya viongozi wa Serikali, waache mara moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Waziri Majaliwa alitoa onyo hilo juzi, tarehe 31 Desemba 2021, akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi.

Waziri Majaliwa aliwataka watu hao wawaheshimu viongozi walioko madarakani, kwani uwepo wao ni mpango wa Mungu.

“Madaraka yote yanatolewa na Mungu,  amepanga kila kitu. Nani atakuwa nani katika kipindi gani,  hata ukilazimisha kutaka nafasi hiyo huwezi kama Mungu hajasema nenda na wala usitumie njia yoyote kumuathiri mwenzako ili apate madhara, eti atoke hapo ili uende hapo,” alisema Waziri Majaliwa.

Waziri Majaliwa alisema ” nani amekwambia utakwenda hapo? Nani amezungumza na Mungu? Tuache tabia ya kuacha viongozi kufanya kazi yao ya kuwahudumia Watanzania na kuwatengenezea migogoro kila siku,  tena mingine ya kusingizia tu.”

Waziri Majaliwa alisema kuwa, wanaotaka kukwamisha viongozi kutekeleza majukumi yao,  hawatafanikiwa.

“Kila nafasi imetengenezwa na Mungu na kila anayekwenda kuongoza Mungu ndiye amesema wewe utakuwa pale. Kama hajasema  hutakuwa, utatumia mihela  mingi itapotea tu,  utakwenda na mambo mengi ya giza  hutadumu. Tuheshimu waliokuwa katika nafasi ya kuwatumikia Watanzania,”

“Uongozi wa sekta yoyote ile unaongozwa na Mungu,  unaweza ukapambana sana ukitaka ukae ukakuta hukai anakaa mwingine,  kwa hiyo utaanza kuathiri wote wanaokaa hapo sababu wewe unataka, wakati Mungu hataki. Lazima tujue kwamba,  madaraka yoyote yanatolewa na Mungu,” alisema Waziri Majaliwa.

Waziri Majaliwa aliwaomba Watanzania wamuombee Rais Samia Suluhu Hassan, ili aendele kutekeleza majukumu yake ya kuiongoza nchi.

“Kwa bahati nzuri rais wetu amekuwa mtumishi serikalini,  anajua kwamba Watanzania wanatamani nini kukiona katika maeneo yao na nyie wote mnajua toka alipoingia madarakani nini amefanya mama mwenye busara na huruma.  Anajua nini anafanya. Watanzania jukumu letu  tuchape kazi sana, hatuna namna ya kumshukuru zaidi ya kuchapa kazi,” alisema Waziri Majaliwa na kuongeza:

“Tumejenga madarasa, tumejitahidi pia kusambaza vituo vya afya kwenye wilaya hii,  tena kimkakati ili watu huduma ya afya iwafuate huko huko. Wana Ruangwa mnataka nini?  Rais ndio huyu anayepitisha mafungu na kila tunachomwambia anasema peleka,  sababu anawapenda wananchi wote.”

1 Comment

  • Asante ndugu majaliwa tumekusikia and wamekuasikia tutafata wako.usia na baadhi yao watajirikebisha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!