Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Waziri Majaliwa akagua ujenzi daraja la Salander, atoa maagizo
Habari Mchanganyiko

Waziri Majaliwa akagua ujenzi daraja la Salander, atoa maagizo

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu,
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amekagua ujenzi wa daraja jipya la Tanzanite (Salander), lililoko jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam…(endelea).

Waziri Majaliwa amekagua ujenzi wa daraja hilo leo Jumanne tarehe 22 Desemba 2020.

Akizungumza katika ukaguzi huo, Waziri Majaliwa ameiagiza Kampuni inayojenga daraja hilo, GS Engineering Corporation ya Korea Kusini,  kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati.

Aidha, Waziri Majaliwa amesema ujenzi wa mradi huo unaendelea vizuri.

Daraja la baharini la Salenda

“Nimekagua mradi na ujenzi wake unaendelea vizuri, sina mashaka na viwango na naamini utakamilika kwa wakati. Watanzania wanasubiri kwa hamu waanze kupita katika daraja hili,” amesema Waziri Majaliwa.

Mkurugenzi wa Miradi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Christianus Ako amesema daraja hilo maarufu kama Salander lenye urefu wa kilomita 1.03 na upana mita 20.5, ujenzi wake unatarajia kukamilika Oktoba 2021.

Mhandisi Ako amesema ujenzi wa daraja hilo unaogharimu Sh  243 bilioni,  una lengo la kupunguza msongamano wa magari kwenye barabara ya Ali Hassan Mwinyi ambayo inatumiwa  na magari mengi yanayoingia na kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo wa miradi TANROADS, amesema hadi kufikia tarehe 30 Novemba 2020, ujenzi wake ulifikia asilimia60.8.

Akieleza faida ya mradi huo, Mhandisi Ako amesema umeajiri wafanyakazi 590, kati yao asilimia 92 ni Watanzania na asilimia nane ni wataalamu kutoka nje ya nchi.

Mhandisi Ako amesema mradi huo unaendelea kutoa mafunzo kwa wahandisi 24 wa Kitanzania kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (5), wahandisi wahitimu (12) na wanafunzi wa uhandisi kutoka vyuo vikuu (7).

“Mafunzo haya yatawajengea uwezo na ujuzi utakaosaidia Taifa hapo baadae,” amesema Mhandisi Ako.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!