Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Jafo aanza kuandamwa 
Habari za Siasa

Waziri Jafo aanza kuandamwa 

Chiku Abwao ambaye ni Mwenyekiti wa Wanawake wa Chama cha ACT-Wazalendo – Taifa
Spread the love

SELEMANI Jafo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), sasa anashinikizwa kujiuzulu. Anaripoti Martini Kamote…(endelea).

Imeelezwa, ni kwa madai ya kushindwa kusimamia uchaguzi wa serikali za mitaa, na kusababisha vyama vya upinzani kuutelekeza kutokana na kuvurugwa na wasimamizi wake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 13 Novemba 2019, Chiku Abwao ambaye ni Mwenyekiti wa Wanawake wa Chama cha ACT-Wazalendo – Taifa amedai, Waziri Jafo anahusika katika kuvuruga uchaguzi.

“Inampasa ajiuzulu, ameshindwa kusimamia uchaguzi, ameamua kupuuza malalamiko ya vyama vyetu na kukibeba chama chake –CCM- kwa kuumiza vyama vyetu.

“Amekuwa akitoa kauli zenye kupingana, huo ni ushahidi tosha kwamba ameshindwa kazi, ili uchaguzi ufanyike kunahitajika usawa ambao chini ya uongozi wake, umeshindwa kupatikana, lakini cha ajabu amekubali kutumika,” amesema.

Amesema, kama uchaguzi huo utafanyika, Wanawake wa ACT-Wazalendo hawatawatambua na wala kutoa ushirikiano kwa viongozi watakaochaguliwa.

“Huu ni uchaguzi wa chama kimoja katika serikali inayojitangaza kuwa na mfumo wa vyama vingi, kati serikali haiwezi kujinasibu kwa kusimamia uchafu huu na kuubariki,” Abwao amemweleza mwandishi wa habari hii.

Amesema, uzoefu unaonyesha kuwa migogoro mingi, hasa ya kutumia nguvu huaathiri zaidi wanawake na watoto kuliko makundi mengine ya jamii.

“Tunawaomba  viongozi wetu wa chama kukutana na vyama vyote makini vya siasa, ili kuwa na msimamo wa pamoja katika hili la kufutwa uchaguzi huu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!