WAZIRI wa Maji nchini Tanzania, Jumaa Aweso ameipa maagizo matatu Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) ikiwemo kudhibiti upagwaji wa gharama za maji bila utaratibu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Aweso amesema hayo leo Ijumaa, tarehe 17 Septemba 2021 jijini Dar es Salaam, wakati akizindua Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Mazingira Dar es Salaam (Dawasa).
Bodi hiyo yenye wajumbe tisa inaongozwa na Jenerali mstaafu Davis Mwamunyange na Katibu wake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Mhandisi Cyprian Luhemeja.
Wakati akizungumza kwenye uzinduzi huo, amempongeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Mhandisi Godfrey Chibulunje kwa kuhudhuria shughuli hiyo na kutumia fursa hiyo kumpa maagizo.
Mosi, Aweso amemtaka Chibulunje kuwa “Lazima uendelee kuwa mkali. Mamlaka inatoza bili ambayo haijaidhinishwa na Ewura tuambie.”
Pili, Waziri Aweso ameitaoa Ewura kuchukua hatua dhidi ya “Mamlaka inayobambika bili tuambie tutashughulika naye. Hatutaki wananchi wabambikiwe bili.”
Mwisho, ameitaka Ewura kufanya “tathimini ya gharama ya uunganishaji wa maji majumbani, serikali inaweka fedha nyingi kwenye miradi. Tunataka kukua Kumuunganishia maji mwananchi ni bei gani.”
“Kama ni gharama kupungua ipungue. Kwa hiyo Ewura ifanyieni kazi hii,” amesema Waziri Aweso
Ameitaka bodi hiyo kuisimamia vyema Dawasa ili iweze kuendeleza kazi nzuri ya kuwafikishia wananchi maji hususan wale wa maeneo ya pembezoni.
Ameipongeza Dawasa kwa kazi nzuri na kuwataka kuongeza kasi zaidi.
Leave a comment