Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee wa Chadema: Muswada wa vyama vya siasa, kaburi la demokrasia
Habari za Siasa

Wazee wa Chadema: Muswada wa vyama vya siasa, kaburi la demokrasia

Hashim Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chadema
Spread the love

MUSWADA wa Vyama vya Siasa waendelea kupingwa na vyama vya upinzani nchi kwa kilichotajwa kuwa kaburi la Demokrasia. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Vyama vya upinzani nchini vimeungana kupinga muswada huo wanaodai kuwa umelenga kuua demokrasia.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Hashim Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chadema amepigilia msumali wa kupinga muswada huo kwa kile alichoeleza umelenga kukipanga nguvu chama tawala na kuua vyama vya upinzani.

“Kuna athari kubwa kwenye nchi hii kukikosekana, sisi tunakosoa Serikali inapokosea,” amesema Juma.

Amesema kuwa Muasisi wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere alikubaliana na mfumo wa vyama vingi kwa sababu alijua kuwa chama tawala kikiwa chenyewe hakitaweza kuwajibika.

Akitoa mfano wa wabunge wa Upinzani walipaza sauti zao kupinga sheria kadhaa ambazo zingekuwa maumivu kwa wananchi amemtaja Ester Bulaya Mbunge wa Bunda Mjini kuwa alipaza sauti yake kuwatetea wastaafu kwenye sheria ya kikokotoo cha asilimia 25 kwenye pensheni ya wastaafu.

Amesema kuwa hakuna mbunge yoyote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyeweza kutetea na kupaza sauti juu ya kikokotoo hiko.

Juma amesema kuwa ifike mahala watanzania wajue umuhimu wa kuwepo kwa wapinzani nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!