Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wazee Ubungo walamba bingo  kutibiwa bure
Habari Mchanganyiko

Wazee Ubungo walamba bingo  kutibiwa bure

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya akitoa kitambulisho cha kupatiwa huduma ya afya bure katika halmashauri ya Ubungo
Spread the love

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amezitaka hosptali za wilaya kuanzisha dirisha  maalum la wazee ili kuwapunguzia changamoto pindi wanapohitaji huduma za matibabu, anaandika Hamisi Mguta.

Waziri Mwalimu ameyasema hayo jana katika Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa matibabu ya bure kwa wazee ambayo itatolewa kwa wazee waishio ndani ya eneo hilo ambao wanafikia 7,299.

Wazee  wamepatiwa vitambulisho vya msamaha wa malipo kwa huduma za afya katika hospitali za serikali.

“Kuwa na vitambulisho ni jambo moja na kupata huduma ni jambo la pili, vitambulisho hivi viwe sehemu ya wazee kupata huduma bora za afya, siyo mzee anaenda na kitambulisho anaambiwa dawa hakuna kanunue, hakutakuwa na ulazima kupatiwa vitambulisho,” amesema

Meya wa Ubungo, Boniface Jacob, amaesema Sh.  1.805 kwa mwaka zitatumika kwa mwaka mmoja ili kuwahudumia  wazee hao kwa vipimo, matibabu na vifaa tiba bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!