Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wazazi, wanafunzi Sekondari Chief Kidulile wamshukuru Rais Samia ujenzi wa madarasa
Elimu

Wazazi, wanafunzi Sekondari Chief Kidulile wamshukuru Rais Samia ujenzi wa madarasa

Spread the love

WAZAZI na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Chief Kidulile wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi na ukarabati wa madarasa katika shule hiyo ambayo huchukua idadi kubwa ya wanafunzi wilayani Ludewa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Hayo yameelezwa na baadhi ya wanafunzi waliozungumza na Mwandishi wetu kuhusu maboresho ya shule hiyo iliyopo katika wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.

Mmoja wa wanafunzi hao, Dorcas Boniphace amesema mazingira ya zamani madarasa waliyokuwa wakiyatumia yalikuwa hayamshawishi mwanafunzi kusoma kwa utulivu.

Amesema muda mwingine wanafunzi walikuwa wanapata shida kupata ufaulu mzuri kwenye masomo kutokana na madarasa yalivyo.

“Milango haikuwepo, ilikuwa unaweza kuingilia mlangoni na kutokea dirishani,” amesema Dorcas na kuungwa mkono na mwanafunzi mwenziye Fadhili Andrew.

Andrew amesema ujio wa madarasa hayo mapya chini ya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan yatawasaidia sana kupandisha ufaulu wao.

“Moja ya sababu ambayo huwa inachangia ufaulu wa wanafunzi ni miundombinu ya shule” amesema.

Aidha, mmoja wa wazazi wa wanafunzi katika Shule hiyo ambayo ipo mjini Ludewa, Monica Mchilo amesema awali walikuwa wanachangishana kujenga madarasa kwa nguvu za wananchi.

“Kwa maana ya matofali, mchanga na mawe lakini ni kweli kwamba kwa nguvu za wananchi tusingeweza kufikia kiwango hiki.

“Tunampoingeza na kumshukuru sana Rais Samia kwa sababu ni mama wa pekee kama waswahili wanavyosema ‘hakuna kama mama’,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!