Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wawili kizimbani kwa kukwepa kodi ya bilioni 6.
Habari Mchanganyiko

Wawili kizimbani kwa kukwepa kodi ya bilioni 6.

Spread the love

 

WANANDUGU wawili, Sibtain Murji 43 na Zameen Murji 47 wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kukwepa kodi kiasi cha Sh. Bilioni sita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa serikali Sylivia Mitanto akisaidiana na wakili Emmanuel Medalakini imedai kuwa tarehe isiyojulikana kati ya Januari 2021 Desemba 2022 jijini Dar es Salaam washtakiwa walishindwa kupeleka tamko la Mapato la biashara iliyosajiliwa kwa jina la Murji Brothers na kupelekea kukwepa kodi ya Sh. 6,224,341983.09/=

Pia inadaiwa, siku na mahali hapo washtakiwa hao kwa pamoja kwa makusudi, walikwepa kodi kwa njia ya udanganyifu na kuisababishia TRA hasara ya kiasi cha fedha zaidi ya Sh. 6 bilioni.


Katika shtaka la utakatishaji fedha inadaiwa, Sikh na mahali hapo washtakiwa hao walijipatia kiasi hicho cha fedha cha sh. bln 6/- huku wakijua kuwa fedha hizo ni zao la kosa tangulizi la kukwepa kodi.

Hata hivyo washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi. Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 3 Machi, 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!