Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Watumishi 139 kada ya afya kusomeshwa ubingwa, ubobezi
Afya

Watumishi 139 kada ya afya kusomeshwa ubingwa, ubobezi

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

 

JUMLA ya watumishi wa afya 139 wamechaguliwa kwaajili ya kupewa ufadhili wa masomo ya ubingwa na ubingwa bobezi katika fani zao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ufadhili huo umetolewa na Serikali kupitia Wizara ya Afya ambapo utatolewa kwa awamu na watumishi 336 watasomeshwa vyuo vya nje ya nchi huku watatu wakisomeshwa katika vyuo vya ndani.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu leo Ijumaa tarehe 28 Oktoba 2022, wakati akitoa taarifa kuhusu mpango wa Serikali wa kuendeleza Watumishi wa Sekta ya Afya katika fani za ubingwa na ubingwa bobezi nchini.

Waziri ummy amesema, Mpango umepewa jina la “Mpango wa Samia wa kuongeza Wataalamu Bingwa na Bobezi wa Afya nchini ” utakao gharimu Sh 8 bilioni.

Aidha, Waziri Ummy amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, kwa kukubali kuongeza fedha kiasi hicho cha fedha zitakazotumika kugharamia wataalamu waliochaguliwa kusoma mafunzo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!