Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko ‘Watu wasiojulikana’ wamuibua  Mkuu wa Majeshi
Habari MchanganyikoTangulizi

‘Watu wasiojulikana’ wamuibua  Mkuu wa Majeshi

Venance Mabeyo, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania. Picha ndogo ni muonekano ya watu wasiojulikana
Spread the love

SAKATA la uvamizi na kupigwa risasi na watu wasiojulikana limemuibua Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Venance Mabeyo ambaye amesema vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi wa matukio hayo, anaandika Mwandishi Wetu.

Hivi karibuni kumekuwa na matukio mabaya ya uhalifu likiwamo la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema),  ambaye amepigwa risasi zaidi ya 30  akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma.

Tukio lingine ni lile la kupigwa risasi, Meja Jenerali mstaafu, Vincent Mribata akiwa nyumbani kwake jambo ambalo limemuibua Jenerali Mabeyo na kutoa kauli nzito.

Amesema watawasaka watu hao na watawakamata wote wanaohusika na vitendo hivyo  vya uhalifu na kuwaomba wananchi kuviachia vyombo vya dola vifanye kazi yao ili vitoe majibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!