Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Watu 400 walazwa hospitalini kwa kung’atwa na nge, watatu wafariki
Kimataifa

Watu 400 walazwa hospitalini kwa kung’atwa na nge, watatu wafariki

Spread the love

 

JUMLA ya watu 400 raia wa Misri wamelazwa hospitalini baada ya kung’atwa na nge na kujeruhiwa katika sehemu mbalimbali za miili yao. Pia hadi sasa jumla ya watu watatu wameripotiwa kupoteza maisha kutokana na wimbi la nge hao ambao wamevamia Mji wa Aswan kusini mwa Misri. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea)

Kwa mujibu wa Gavana wa mji huo wa Aswan, Ashraf Attia amesema baadhi ya maeneo watu wamevamiwa na nge baada ya dhoruba za mvua na mchanga kufukua makundi ya nge wenye sumu na kuwashambulia raia.

Kwa kawaida mvua kubwa ikinyesha nchini humo nge husombwa kutoka kweye maficho yao na kuzagaa mtaani kama ilivyo kwa nyoka, ambao pia husombwa na maji kutoka kwenye mashimo yao.

Hospitali na vituo vya matibabu vya Aswan vimejaa wagonjwa walioumwa na nge hao wenye sumu.

Mji wa Aswan kusini mwa Misri ndio ulioathirika zaidi na uvamizi wa nge hao, ambapo mvua kubwa ya mawe pamoja na radi katika eneo karibu na Mto Nile ilishuhudiwa siku ya Ijumaa tarehe 12 Novemba, 2021.

Watu wamehimizwa kupunguza kutembea mitaani na kukaa kwa tahadhari majumbani pamoja na kuepuka maeneo yenye miti mingi.

Aidha, Gavana Attia ametangaza masharti ya watu kutosafiri katika mji huo kutokana na hali ya hewa ya mvua kubwa na ukungu unaosababisha madereva kutoona vizuri.

Mamlaka nchini humo zimechukua hatua ambapo mpaka sasa dozi za ziada za kuzuia sumu zimetolewa kwa vituo vya matibabu katika vijiji vilivyo karibu na milima na jangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!