Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watu 13 wafikishwa mahakamani kwa uhujumu uchumi
Habari za Siasa

Watu 13 wafikishwa mahakamani kwa uhujumu uchumi

Spread the love

WATU 13 wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwemo utakatishaji fedha wa Sh. 154 milioni. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akiwasomea mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Kelvin Mhina wakili wa serikali mkuu, Nassoro Katuga amedai kuwa washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 5 ambayo wameyatenda katika mikoa tofauti.

Katika kosa la kwanza la kula njama ya kutenda kosa linawakabili washtakiwa wote ambapo wanadaiwa wamelitenda kati ya March 2018 na June 2018 katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Rukwa na katika maeneo mengine ya jamhuri ya Tanzania.

Pia kosa jingine ni kusambaza taarifa za uongo kupitia mfumo wa kompyuta ambapo wanadaiwa wamelitenda March na June 2018 wakiwa Dar es Salaam na Rukwa ambapo walichapisha taarifa za ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) ili kujipatia kipato.

Wakili Katuga amedai kosa jingine ni kusambaza jumbe (message) kwa njia ya Elektroniki kati ya March na June, 2018 kwa nia ya kudanganya na kushawishi kati ya Dar es Salaam na Rukwa walisambaza kwenda kwa watu tofauti tofauti ili kuonyesha wana mamlaka hayo.

Pia katika kosa jingine la kusambaza jumbe fupi za Kielektroniki, wanadaiwa walilitenda March na June, 2018 kati ya Dar es Salaam na Rukwa walisambaza jumbe zisizotakiwa kwa njia ya Kielektroniki.

Katika kosa la mwisho wanadaiwa ni utakatishaji fedha ambapo wanadaiwa wamelitenda kati ya March na June 2018 katika maeneo ya Dar es Salaam na Rukwa.

Inadaiwa kwa pamoja walijihusisha katika ufanyaji wa muamala wa Sh.Mil 154,032,830 ikiwa ni zao la kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, wakili Katuga amedai upelelezi haujakamilika ambapo Hakimu Mhina amesema kesi hiyo haina dhamana kwa sababu ni ya uhujumu uchumi, hivyo wataenda lumande ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi August 21,2018.

Katika kesi hiyo washtakiwa Boniface Maombe, David Luvanda, Moshi Sungura, Amos Bosco, Lule Kadenge, Jofrey Kapangamwaka, William Nturo, Regius Mauka, Collins Basham, Francis Kapalata, Kasonde Kapela, Enock Mwandaji na Pascal Kiatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!