
WATU 10 ikiwemo wanafunzi wanane, wamefariki dunia huku 17 wakijeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Mji Mwema, mkoani Mtwara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).
Taarifa ya ajali hiyo iliyotokea mapema leo Jumanne, tarehe 26 Julai 2022, imetolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mtwara, ACP Nicodemus Katembo, akizungumza na wanahabari.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda Katembo, watoto watano kati ya majeruhi 17, wako katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), huku wengine wakiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Ligula.
Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa Shule ya Msingi King David na watu wazima wawili vilivyotokea leo eneo la Mjimwema, Mikindani, mkoani Mtwara. Natoa pole kwa wote waliopoteza jamaa zao. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema na awajalie majeruhi wapone haraka.
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) July 26, 2022
Chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa ni kufeli kwa mfumo wa breki wa gari lililokuwa limebeba wanafunzi hao kutoka Shule ya Msingi ya King David na wa shule jirani.
Akizungumzia ajali hiyo, Mkuu wa Shule ya Msingi ya King David, amesema kati ya wanafunzi wanane waliofariki dunia, watano ni wanafunzi wa shule yake pamoja na dereva.
More Stories
Mikoa yatakiwa kutenga maeneo makubwa ya kilimo
Mtendaji Ruaha asimulia njama za kutaka kumuua zilivyopangwa
Samia: Vijana njooni kwenye kilimo