Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watoto wa Rungwe wapatikana
Habari za Siasa

Watoto wa Rungwe wapatikana

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chama cha Umma
Spread the love

WALE watoto wa Mzee Hashim Rungwe akiwemo mpwa wake wa kike, waliokuwa hawaonekani kwao, “wameachiwa.” Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rungwe, mfanyabiashara mkubwa nchini na kiongozi wa Chama cha Umma, amesema vijana hao wamerudi nyumbani.

“Aah… wamewaachia. Naona wameturidhia na kutusikiliza,” ni maneno machache aliyoyatoa punde hivi kwa Mhariri wa MwanaHALISI, Jabir Idrissa, kwenye vipenu vya Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.

“Wamewaachia tayari. walikuwa nao huko,” alikazia kauli yake. Hakueleza zaidi mazingira ya kupatikana kwa watu wake,” amesema Rungwe.

Rungwe ni wakili wa kujitegemea nchini na amefika Mahakama ya Kisutu kikazi.

Aliulizwa na Idrissa baada ya kuchomoza ghafla mahakamani Kisutu ambako Mhariri alikwenda kuhudhuria kesi ya tuhuma za uchochezi kuhusu alichokiandika katika gazeti la MAWIO Januari mwaka juzi.

Kesi hiyo iliyokwama kusikilizwa kwa sababu ya kutokuwepo kwa Tundu Lissu ambaye ni mtuhumiwa wa nne, inawahusu pia Simon Mkina, Mhariri Mtendaji na Ismail Mehboob Meneja wa kiwanda cha uchapaji magazeti cha Flint.

Kwa mara nyingine leo kesi hiyo imetajwa na kuahirishwa kwa ombi la upande wa mashtaka ambao unaeleza mtuhumiwa Lissu yuko nje ya nchi anaumwa.

Wakili wa Serikali ameiambia mahakama leo kuwa wanawasiliana na DPP ili “kuona njia nzuri ya kufanya kumaliza shauri hili.”

Hakimu Thomas Simba alisema hiyo ni hatua nzuri kufuatwa kwani kesi ina mazingira yanayoelezeka. Itatajwa tena tarehe 30 Aprili mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!