Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Watoto wa Rungwe wapatikana
Habari za Siasa

Watoto wa Rungwe wapatikana

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chama cha Umma
Spread the love

WALE watoto wa Mzee Hashim Rungwe akiwemo mpwa wake wa kike, waliokuwa hawaonekani kwao, “wameachiwa.” Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rungwe, mfanyabiashara mkubwa nchini na kiongozi wa Chama cha Umma, amesema vijana hao wamerudi nyumbani.

“Aah… wamewaachia. Naona wameturidhia na kutusikiliza,” ni maneno machache aliyoyatoa punde hivi kwa Mhariri wa MwanaHALISI, Jabir Idrissa, kwenye vipenu vya Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.

“Wamewaachia tayari. walikuwa nao huko,” alikazia kauli yake. Hakueleza zaidi mazingira ya kupatikana kwa watu wake,” amesema Rungwe.

Rungwe ni wakili wa kujitegemea nchini na amefika Mahakama ya Kisutu kikazi.

Aliulizwa na Idrissa baada ya kuchomoza ghafla mahakamani Kisutu ambako Mhariri alikwenda kuhudhuria kesi ya tuhuma za uchochezi kuhusu alichokiandika katika gazeti la MAWIO Januari mwaka juzi.

Kesi hiyo iliyokwama kusikilizwa kwa sababu ya kutokuwepo kwa Tundu Lissu ambaye ni mtuhumiwa wa nne, inawahusu pia Simon Mkina, Mhariri Mtendaji na Ismail Mehboob Meneja wa kiwanda cha uchapaji magazeti cha Flint.

Kwa mara nyingine leo kesi hiyo imetajwa na kuahirishwa kwa ombi la upande wa mashtaka ambao unaeleza mtuhumiwa Lissu yuko nje ya nchi anaumwa.

Wakili wa Serikali ameiambia mahakama leo kuwa wanawasiliana na DPP ili “kuona njia nzuri ya kufanya kumaliza shauri hili.”

Hakimu Thomas Simba alisema hiyo ni hatua nzuri kufuatwa kwani kesi ina mazingira yanayoelezeka. Itatajwa tena tarehe 30 Aprili mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!