Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Watengenezaji vinywaji vya Energy waonywa
Habari Mchanganyiko

Watengenezaji vinywaji vya Energy waonywa

January Makamba, Waziri wa Nishati
Spread the love

JANUARI Makamba, Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mazingira na Muungano ametoa angalizo kwa watengenezaji wa vinywaji vya Enegy kwamba, chupa zake hazidhibitiki. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 29 Aprili 2019 amesema, takataka aina ya chupa zimekuwa ni ajira kwa waokotaji na kuwa, serikali imepanga kurasimisha shughuli hiyo lakini chupa za Energy hazinunuliki.

Amewataka watengenezaji wa chupa za vinywaji hivyo kutafute namna ya kuzifanya ziwe kwenye mzunguko wa kutoka kwenye mazingira kama takataka.

“Washiriki kuziondoe katika mazingira, wewe unatengeneza Enegy Drink ukaamua kuzipiga rangi, hujui chupa inakwenda wapi na halafu hujui namna ya ile chupa inaweza kurudishwa,” amesema Makamba.

Amesema kuwa, serikali inajianda kisera kuhakikisha kuwa, takataka zinakuwa mali zenye kutoa fursa ya kiuchumi nchini.

Akizungumzia fursa itokanayo na takataka za chupa amesema kuwa, imetoa ajira kwa watu wanaoziokota na kwenda kuuza ambapo serikali imepanga kuwatambua rasmi watu hao.

“Watu wanakusanya taka tunaona wanazunguka na wakati mwengine tunawaona kama vichaa kwasababu wanaokota makopo, lakini ile ni shughuli ya kipato, sisi tunaona irasimishwe.

“Miji mingi dunini na hata hapa kwetu, kulingana na shughuli za uchumi, uzalishaji taka unazidi kukua hivyo serikali tunalitazama hilo kwenye kutengeneza mifumo ya kuzifanya kuwa mali.” amesema.

Na kwamba, mfumo wa utupaji wa taka na urejeshaji wake ni muhimu ukapangiliwa ili kuleta manufaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!