Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wateja NHIF kutambuliwa kwa sura, alama za vidole
Habari Mchanganyiko

Wateja NHIF kutambuliwa kwa sura, alama za vidole

Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga
Spread the love

 

KATIKA kurahisisha utambuzi wa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika vituo vya kutolea huduma na kudhibiti vitendo vya udanganyifu, Mfuko umejipanga kuanza kutumia Mfumo wa kuwatambua wanachama wake kwa kutumia sura na alama za vidole. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hatua hizo zimeelezwa leo Alhamisi tarehe 23 Februari 2023 na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga, katika mkutano wa Waganga Wakuu wa Mikoa, Waganga Wakuu wa Wilaya na Waganga Wafawidhi wa Vituo nchini unaofanyika Mkoani Dodoma.

“Ili kwenda na kasi ya ongezeko la idadi ya wanachama katika kuwahudumia kwa haraka, kulipa kwa wakati madai ya watoa huduma na wingi wa vituo, Mfuko unalazimika sasa kuhakiki wanachama wake kwa kutumia sura na alama za vidole,” amesema Konga.

Aidha amesema kuwa uwasilishaji, uchakataji na ulipaji wa madai utafanyika kwa njia ya Kielektroniki (e-Claims and online submission) ambapo itasaidia kupunguza matumizi ya fomu.

Pia amesema madai yatalipwa kwa njia ya kielektroniki moja kwa moja katika akaunti za vituo (e- Claims Payment) ili kuondoa malalamiko ya ucheleweshaji wa madai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!