Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania wawili mbaroni kwa kumtumia mlemavu kuombaomba Nairobi
Habari MchanganyikoKimataifa

Watanzania wawili mbaroni kwa kumtumia mlemavu kuombaomba Nairobi

Spread the love

 

WATANZANIA wawili wamepandishwa kizimbani kwa wakikabiliwa na mashtaka ya kumtumia mlemavu kujitajirisha kupitia kwa kuombaomba katika barabara za jijini Nairobi nchini Kenya. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Washtakiwa hao, Kuyi Paulo na Sita Yohana walifikishwa katika Mahakama ya Milimani Jumatatu tarehe 30 Agosti, 2021 wakituhumiwa na ulanguzi wa binadamu.

Kwa mujibu wa  vyombo vya habari nchini humo, wawili hao pia wanaripotiwa kumpokonya mlemavu huyo pesa alizokuwa anaombaomba barabarani jijini Nairobi.

Hata hivyo, wawili hao walikanusha shtaka la kukiuka haki za mlalamikaji huyo mwenye umri wa miaka 14.

Mahakama pia ilifahamishwa kuwa wawili hao walikandamiza haki ya mlalamishi kwa kumnyima fursa ya kupata elimu ili wajikimu kiuchumi.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Milimani, Zainab Abdul alielezwa na Kiongozi wa Mashtaka, Everlyn Ongunga kuwa wawili hao walikuwa wakimsafirisha mlemavu huyo kila siku katika mtaa Shauri Moyo, Nairobi kuomba kando ya barabara.

Hakimu Abdul aliwashurutisha wawili hao kulipa dhamana ya Sh milioni 6.3 pesa taslimu kila mmoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!