
Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima
WIZARA ya Fedha imesema hakuna madai yoyote ambayo Serikali inadaiwa na wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyovunjika.
Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima amelieleza Bunge wakati akijibu swali la Mbunge wa Lindi Mjini, Salum Barwany (CUF).
Barwany alitaka kujua serikali inatoa kauli gani kwa wastaafu hao ambao baadhi yao hawajalipwa kabisa huku wengine wakilipwa kiwango cha chini sana bila kuzingatia hali halisi ya uchumi.
Katika majibu yake, Malima amesema,”wazee hao wamelipwa mafao yao kwa mujibu wa hati ya makubaliano, hakuna madai mengine ambayo serikali inadaiwa.”
Amesema hadi 31 Desemba 2013, serikali imewalipa wastaafu 31,792 ambapo zilitumika Sh. 117 bilioni.
More Stories
Mrithi wa Maalim Seif, siri nzito
Rais Magufuli amuapisha Katibu Mkuu Kiongozi mpya
Dk. Bashiru: Nilipata taarifa za uteuzi mitandaoni