Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wasomi wananiangusha – Rais Magufuli
Habari za Siasa

Wasomi wananiangusha – Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ameeleza kusikitishwa na wasomi anaowateua kwenye nafasi mbalimbali kwamba, wengi wao wanamwangusha. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Mei 2019, wakati akihutubia kwenye halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST).

Kiongozi huyo wan chi ametoa kauli hiyo, baada ya uongozi wa MUST kulalamika kwamba, Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imechelewa kutoa hati ya ithibati kwa chuo hicho.

Kufuatia malalamiko hayo, Rais Magufuli ameshangazwa na ucheleweshwaji huo, akisema kwamba, haiwezekani chuo hicho kikose hati ya ithibati wakati watendaji wa mamlaka husika ambao ni TCU iliyochini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknlojia kuna viongozi waliosoma.

“Mi najitahidi kuchagua wasomi nao wananiangusha na wote wako kwenye wizara moja, waziri aliyepo ni profesa, TCU iko chini ya wizara yake, hawa wanalalmika TCU hawatoi waziri upo.

“Sasa natoa siku 10 majibu yawe yametolewa kama ni ndio au hapana, sasa ninaomba waziri shughulikia. TCU washughulikie ithibati mahala pengine wasicheleweshe tunajichelewesha sisi wenyewe,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ametoa siku 10 kwa Mwenyekiti wa Bodi ya TCU, Profesa Philip Mtabaji pamoja na watendaji kufika chuoni hapo kwa ajili ya kushughulikia changamoto hiyo.

“Mwambie Prof. Mtabaji ndani ya siku 10 awe ameshakuja hapa pamoja na watendaji wake. Ninajua mnanisikia, wajadili kuhusu suala la ithibati.

“Hawezekani changamoto kwamba, TCU huchelewa sana kutoa hati ya ithibati mliomba mpate hiyo hati tangu mwaka 15 aliyepo hapa ni profesa mwenzake anayetakiwa kutoa kibali ni profesa,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!