Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Washereheshaji wawakumbuka watoto yatima, wafungwa
Habari Mchanganyiko

Washereheshaji wawakumbuka watoto yatima, wafungwa

Spread the love

MARAFIKI wa Mshehereshaji (MC) Mwangata Fomma wametoa msaada kwa kuwalipia kadi za bima ya afya kwa watoto nane wa Kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu na yatima cha Masisita wa Mt. Urusula kilichopo Miyuji Jijini Dodoma.

Pia wametoa msaada wa magodoro 20 kwa wafungwa wa Gereza la Isanga ambapo magodoro 10 watapewa wafungwa wanawake na 10 watapewa wafungwa wanaume. Anaripoti Danson Kaijage …(endelea).

Msaada huo umetolewa leo tarehe 19 Machi, 2022 na kwa lengo la kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha mwaka mmoja aliotimiza akiwa madarakani.

Akizungumzia msaada huo mmoja wa marafiki hao wa MC Mwangata, Naterius Lukinjason amesema umoja huo pia umetoa misaada ya sukari, mafuta ya kupaka kwa watoto hao wa kituo hicho cha kulelea watoto.

Aidha, akitoa neno la shukrani Msaidizi wa kituo, Sista Elizabeth Mtema amewashukuru wana umoja huo kwa kuona umuhimu wa kutoa sadaka kwa watoto hao.

“Kwa niaba ya mkuu wa kituo hiki Alizea Kyara, nipende kuwashukuru kuwapatia baadhi ya watoto bima za afya na misaada mingine ya chakula na mafuta.

“Kituo kina jumla ya watoto 62 na kwa sasa wapo watoto 36 kwa kuwa wapo watoto ambao wapo katika vyuo mbalimbali,” amesema.

Aidha, amesema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa chakula baada ya wafadhili kuzeeka pamoja na kushuka kwa uchumi kutokana na kuwepo kwa changamoto ya ugonjwa wa uviko-19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!