Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Maisha Burudika Wasanii wapewa neno kuondokana na aibu
Burudika

Wasanii wapewa neno kuondokana na aibu

Jimmy Mafufu, Makamu  Mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji Tanzania
Spread the love

MAKAMU  mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji Tanzania, Jimmy Mafufu amewataka wasanii kujiunga katika mfumo wa bima kupitia mfuko wa PPF ili kuondokana na aibu za kuchangishana fedha kupitia vyombo vya habari wakati wa matatizo, anaandika Hamis Mguta.

Mafufu amesema kuwa lengo la mfuko wa PPF ni kusaidia watanzania, lakini wameona wasanii pia wana matatizo mengi.

“Watu hawana bima za afya, wanaumwa wanachangishana kwenye TV, ni aibu sana kuona msanii anaumwa harafu Radio, Magazeti na TV zinaandika achangishiwe pesa,” amesema Mafufu.

Amesema kuwa tarehe 14 Octoba mwaka huu, waigizaji, waaandaaji wa filamu wadau na watanzania wote watatakiwa kufika katika viwanja vya posta jijini Dar es Salaam ili kujiunga katika mfuko huo.

“Kupitia PPF waigizaji tunakwenda kupata sifa za kukopesheka na dhamana yako ni mchango uliochangia tu, kujiunga ni hure lakini kila mwisho wa mwezi mtu ambaye anajiunga atalipa Sh 20,000,” amesema.

Mtazame kwenye video hii…

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BurudikaMichezo

Kizz Daniel aunguruma na EP mpya ‘Thankz alot’

Spread the loveMKALI wa muziki nchini Nigeria, Kizz Daniel ametoa EP yake...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Burudika

Piga makofi kwa Mr. Eazi …achomoka na ‘The Evil Genius’

Spread the loveMAKOFI kwa Mr Eazi! Staa wa Afropop, Mr Eazi ameachia...

Burudika

Kishindo cha Afro B katika “Wo wo wo” akiwa na Rich the Kid&Rimzee

Spread the loveSTAA ambaye alitambulishwa na ngoma maarufu, Afrowave ‘Drogba’, Afro B,...

error: Content is protected !!