Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Michezo Wapinzani wa Simba kucheza na Bayern Munich
Michezo

Wapinzani wa Simba kucheza na Bayern Munich

Al Ahly
Spread the love

 

WAPINZANI wa Simba kwenye Michuano ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly kutoka Misri wanatarajia kuvaana na FC Bayern Munich kutoka Ujerumani kwenye hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa Dunia. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Al Ahly ambayo ipo kwenye kundi A, ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika sambamba na Simba kutoka Tanzania, AS Vita ya Congo DR na El Merreikh kutoka nchini Sudan.

Klabu hiyo inashiriki michuano hiyo ikiwa kama bingwa ndani ya bara la Afrika, ambapo mara baada ya michuano hiyo itarudi tena kuanza tena mbio za kutetea taji hilo dhidi ya El Merreikh ya Sudan na tarehe 23 Februari 2021 itaikabili Simba kwenye uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam

Bao pekee la Al Ahly kwenye mchezo wa jana dhidi ya Al Duhail ya Qatar, lilifungwa na El Shahati kwenye dakika ya 30.

Ushindi huo utawafanya mabingwa hao wa Afrika kwa msimu wa 2019/20, kukutana na mabingwa Ulaya klabu ya Bayern Munich kwenye mchezo wa nusu fainali utakaopigwa tarehe 8 Februari 2021.

1 Comment

  • Al~ahaly ya misri hizii ndio timu nzuri zakushabikiaa sio majanga kama hizi timu za kurithii zahapa bongoo!!!!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!