Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Wapinzani Uganda wala ‘kibano’ kama wa Tanzania
Kimataifa

Wapinzani Uganda wala ‘kibano’ kama wa Tanzania

Askari Polisi nchini Uganda wakiwa katika majukumu yao ya kawaida
Spread the love

POLISI nchini Uganda imewatia mbaroni wapinzani waliofanya mkusanyiko wa kupinga serikali wiki iliyopita, anaandika Hellen Sisya.

Emilian Kayima, Msemaji wa jeshi la polisi nchini humo amesema kuwa, karibu wapinzani 20 wa kundi moja la upinzani akiwemo kiongozi wa kundi hilo, walitiwa mbaroni siku ya jana kwa tuhuma za kufanya mkutano kinyume cha sheria.

Kayima ameongeza kuwa, watu wengine 56 walitiwa mbaroni siku ya Jumatano kwa kuhusika na tuhuma hiyo.

Wapinzani nchini humo wamekuwa wakifanya maandamano ya kupinga kile wanachosema kuwa ni njama za Rais Yoweri Museven wa taifa hilo za kutaka kubadili katiba kwa lengo la kubakia zaidi madarakani, ingawa yeye mwenyewe amekuwa akikanusha tuhuma hizo.

Alhamisi ya jana wapinzani walitia saini tambara la maoni katika kulalamikia mpango wa serikali wa kuifanyia mabadiliko katiba ya Uganda kwa lengo la kuondoa ukomo wa umri kwa rais wa nchi hiyo.

Katika katiba ya sasa kumeainishwa mpaka na umri wa miaka 75 kwa ajili ya urais. Kwa sasa Rais Yoweri Museven ana umri wa miaka 72 akiwa madarakani tangu mwaka 1986 na kwa mujibu wa katiba nchi hiyo Museven anatakiwa kuondoka madarakani ifikapo mwaka 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!