Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanne mbaroni tuhuma za kuhujumu miundombinu ya reli
Habari Mchanganyiko

Wanne mbaroni tuhuma za kuhujumu miundombinu ya reli

Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara, SACP Mwamini Rwantale
Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini Tanzania kupitia Kikosi cha Polisi cha Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara), linawashikilia watu wanne, kwa tuhuma za kuiba vyuma vya miundombinu ya reli mkoani Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Jumanne, tarehe 17 Agosti 2021 na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara, SACP Mwamini Rwantale, akizungumzia doria ya kudhibiti vitendo vya hujuma kwenye miundombinu ya reli ya shirika hilo, kuanzia Dar es Salaam, hadi Tunduma mkoani Songwe.

Waliokamatwa kufuatia tuhuma hizo ni, Bakari Mussa (54), mkazi wa Yombo, ambaye ni mfanyabiashara na Abraham Emmanuel (35), mlinzi na mkazi wa Buguruni.
Wengine ni, fundi wa kuchomelea vyuma, Frank Jerome (32), mkazi wa Temeke na Waziri Alli (25), dereva wa pikipiki ‘Bodaboda’.

Kamanda Rwantale amesema, watuhumiwa hao walikamatwa tarehe 4 Agosti 2021, maeneo ya Vertinaly Temeke, mkoani Dar es Salaam.

“Kupitia doria na misako, kikosi kimefanikwa kuwakamata watu wanne kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu ya reli. Walikamatwa watuhumiwa hao eneo la vertinaly Temeke, wakiwa na vyuma mbalimbali vya miundombinu ya reli,” amesema Kamanda Rwantale.

Amesema Watuhuma wote watafikishwa mahakamani hivi karibuni kujibu tuhuma zinazowakabili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!