ZAIDI ya wanawake na watoto 60 waliotekwa nyara wiki iliopita na watu wanaoshukiwa kuwa ni wanajihadi, huko kaskazini mwa Burkina Faso wameachiliwa huru. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Vikosi vya usalama nchini humo viliendesha oparesheni ya uokoaji wa kundi hilo la watu na kuwapata wanawake 27 watoto na wasichana wapatao 39, jirani na jimbo la kati ya Kaskazini.
Mamlaka nchini humo ilisema mapema wiki hii kwamba wahanga hao walitekwa nyara wakiwa katika shughuli za utafutaji matunda pori na vyakula vingine.
Tukio la utekaji nyara wa idadi kubwa ya watu nchini humo haujawahi kushuhudiwa licha ya taifa hilo la Afrika Magharibi kukabiliwa na uasi uliokithiri wa itikadi kali uliofungamana na makundi ya dola la kiislam na Al-Qaeda ambao umeenea nchi jirani ya Mali tangu 2015.
Leave a comment