Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanawake, watoto 60 waliotekwa waachiwa huru
Kimataifa

Wanawake, watoto 60 waliotekwa waachiwa huru

Spread the love

 

ZAIDI ya wanawake na watoto 60 waliotekwa nyara wiki iliopita na watu wanaoshukiwa kuwa ni wanajihadi, huko kaskazini mwa Burkina Faso wameachiliwa huru. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Vikosi vya usalama nchini humo viliendesha oparesheni ya uokoaji wa kundi hilo la watu na kuwapata wanawake 27 watoto na wasichana wapatao 39, jirani na jimbo la kati ya Kaskazini.

Mamlaka nchini humo ilisema mapema wiki hii kwamba wahanga hao walitekwa nyara wakiwa katika shughuli za utafutaji matunda pori na vyakula vingine.

Tukio la utekaji nyara wa idadi kubwa ya watu nchini humo haujawahi kushuhudiwa licha ya taifa hilo la Afrika Magharibi kukabiliwa na uasi uliokithiri wa itikadi kali uliofungamana na makundi ya dola la kiislam na Al-Qaeda ambao umeenea nchi jirani ya Mali tangu 2015.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!