MBIO za kuwania Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020 zinazidi kushika kasi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya mwanamke wa tatu kujitoka kwenye harakati hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).
Tangu shughuli ya uchukuaji na urejeshaji fomu ilipoanza tarehe 15 hadi 30 Juni 2020 imeshuhudia viongozi waliopo madarakani kama mawaziri, wakuu wa mikoa na watoto wa Marais wastaafu wa Zanzibar wakijitosa kwenye mbio hizo.
Leo Jumatano tarehe 24 Juni 2020, Fatma Kombo Masound amekuwa mwanamke wa tatu kuchukua fomu kuwania kumrithi Rais Ali Momahed Shein, ambaye anamaliza muda wake wa uongozi wa miaka 10.
Wanawake wengine waliojitosa kwenye kinyang’anyiro hicho ambacho wagombea wamefikia 26 ni; Hasna Atai Masound aliyechukua fomu mapema leo Jumatano asubuhi na Mwatum Mussa Sultan.
Mara baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Fatma aliwaeleza waandishi wa habari kwamba hana la kuzungumza na apewe fursa ya kwenda kuzisoma fomu hizo kujua anapaswa kufanya nini.
Wengine 25 waliokwisha kuchukua fumo ni;
- Mbwana Bakari Juma
- Ali Abeid Karume
- Mbwana Yahya Mwinyi :
- Omar Sheha Mussa
- Hussein Ali Mwinyi
- Shamsi Vuai Nahodha
- Mohammed Jaffar Jumanne
- Mohammed Hijja Mohammed
- Issa Suleiman Nassor
- Makame Mnyaa Mabarawa
- Mwatum Mussa Sultan
- Haji Rashid Pandu
- Abdulhalim Mohammed Ali
- Jecha Salum Jecha
- Dk Khalid Salum Mohammed
- Rashid Ali Juma
- Khamis Mussa Omar
- Mmanga Mjengo Mjawiri
- Hamad Yussuf Masauni
- Mohammed Aboud Mohammed
- Bakari Rashid Bakari
- Hussein Ibrahim Makungu
- Ayoub Mohammed Mahmoud
- Hashim Salum Hashim
- Hasna Atai Masound
Leave a comment