Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanawake wamkabidhi changamoto sita Rais Samia
Habari za SiasaTangulizi

Wanawake wamkabidhi changamoto sita Rais Samia

Spread the love

 

WANAWAKE wa Mkoa wa Dodoma, wamemkabidhi changamoto sita Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, wakimuomba azitatue ili kuleta ustawi wa kundi hilo nchini. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Changamoto hizo zimetolewa leo Jumanne, tarehe 8 Juni 2021 na Joyce Kashozi, akisoma risala ya wanawake hao, katika mkutano wao na Rais Samia, uliofanyika jijini Dodoma.

Kashozi ametaja changamoto hizo ni, ukosefu wa maji safi na salama katika baadhi ya maeneo hasa ya vijijini, ukosefu wa fedha za kutosha za mikopo inayotolewa na halmashauri na upungufu wa watalaamu, vifaa tiba na miundombinu ya sekta ya afya.

Nyingine ni, upungufu wa walimu na miundombinu ya sekta ya elimu na ombwe la wanawake katika nafasi za uongozi na kwenye vyombo vya utoaji maamuzi.

Akisoma risala hiyo, Kashozi amesema changamoto hizo zinarudisha nyuma maendeleo ya wanawake, na kwamba zinapaswa kutafutiwa ufumbuzi.

“Changamoto hizi ikiwemo uwiano usiolingana kati ya wanawake na wanaume, katika nafasi mbalimbali za uongozi na ufanyaji maamuzi, mila na desturi potofu zinazokandamiza wanawake, zikitatuliwa zitaleta ustawi wa wanawake nchini,” amesema Kashozi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!