Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanasiasa, msajili na IGP Sirro kukutana Oktoba 21
Habari za SiasaTangulizi

Wanasiasa, msajili na IGP Sirro kukutana Oktoba 21

Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi
Spread the love

 

MKUTANO wa wadau wa vyama nchini Tanzania, unatarajiwa kufanyika tarehe 21 Oktoba 2021, jijini Dodoma. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo ilitolewa jana Jumatatu tarehe 20 Septemba 2021 na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, kuhusu ratiba ya mkutano huo wa wadau.

Jaji Mutungi alisema, mkutano huo utakutanisha wadau wa siasa, ikiwemo Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro na wawakilishi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), ambao utaongozwa na mtu asiyekuwa na upande wowote, ili kuweka usawa.

“Kikao cha wadau kikiendeshwa na IGP kinaweza leta taswira IGP huyo huyo ndiyo tunamlalamikia, kikiendeshwa na msajili, msajili huyo huyo tuna madudu yake tunataka kuyasema, mwenyekiti wa uendeshaji kikao atakuwa mtu neutral,” alisema Jaji Francis.

Simon Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP)

Msajili huyo wa vyama vya siasa alisema, kikao hicho kitasaidia kupatikana kwa muafaka wa vikwazo, vinavyokabili wadau wa siasa na demokrasia nchini.

“Naamini huu mlolongo tuliyouweka utavuka vikwazo vyote, ambavyo vilifikirika kwamba vitakwamisha muafaka mzuri tunaotaka upatikane na nieleweke vizuri, ninaposema muafaka kuna vitu ambavyo kama viko kisheria hakuna suala la muafaka si sheria ipo?” alisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi alisema “lakini sisi tunataka kuangalia kama sheria ipo, lakini sisi tunataka tuangalie kama sheria ipo halafu bado kuna misuguano tatizo liko wapi. Ndiyo mantiki ya watu kukaa meza moja kuelewana.”

“Umuhimu wa kukaa ndiyo dhana nzima ya demokrasia, tunapofika mahala tukajaribu kuona kwamba hapa mbona kuna sintofahamu, inawezekana ni sintofahamu ya kuelimishana tu, ya kueleweshana,” alisema Jaji Mutungi.

John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema

Jaji Mutungi alisema mkutano huo wa wadau utatanguliwa na vikao mbalimbali, ikiwemo kikao cha ofisi yake na Jeshi la Polisi, kitakachofanyika jijini Dodoma, tarehe 23 Septemba 2021, kikifuatiwa na kikao cha Kamati ya Uongozi ya Baraza la Vyama vya Siasa, kitakachofanyika tarehe 30 Septemba 2021.

“Tutakaa na na Polisi halafu tutaitisha kamati ya uongozi ya baraza, sababu imeonekana tusiongee tu na Polisi na wanasiasa tuwape kikao maalum, wakae warasimishe hoja ambazo ndizo zinazosemekana au ndizo walizonazo zinazohusiana na suala nzima la hiyo sintofahamu, tuliyokuwa tunajaribu kuisema,” alisema Jaji Mutungi.

Jaji Mutungi alisema kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa, kitafanyika tarehe 13 Oktoba 2021, visiwani Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!