Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanaompinga Rais Mnangagwa watoswa Zimbabwe
Kimataifa

Wanaompinga Rais Mnangagwa watoswa Zimbabwe

Spread the love

MAHAKAMA ya Kikatiba nchini Zimbabwe imetupilia mbali maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na chama kikuu cha upinzani nchini humo MDC, ya kukata rufaa dhidi ya matokeo ya uchaguzi wa urais yaliyomuweka madarakani Rais Emmerson Mnangagwa. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Chama Kikuu cha Upinzani nchini Zimbabwe, MDC kikiongozwa na aliyekuwa mgombea wake wa urais katika uchaguzi uliofanyika wiki kadhaa zilizopita, kilikwenda mahakamani kupinga matokeo hayo kikidai kuwa yalilenga kumpendelea Rais Mnangagwa.

Uamuzi huo wa mahakama ulitolewa na Jaji Mkuu, Luke Malaba leo Ijumaa tarehe 24 Agosti, 2018 baada ya MDC kushindwa kuithibitishia mahakama hiyo kuhusu udanganyifu uliofanyika kwenye uchaguzi huo.

Katika uchaguzi huo, Rais Mnangagwa kutoka chama tawala cha ZANU-PF alishinda kwa ushindi mwembamba wa asilimia 50.8 ya kura huku aliyekuwa mpinzani wake wa karibu Chamisa akiambulia asilimia 44.3 ya kura wakati asilimia zilizosalia zikichukuliwa na wagombea wa vyama vingine walioshiriki uchaguzi huo wa urais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!