Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wananchi wafungiwe dira mpya za maji – Serikali
Habari za Siasa

Wananchi wafungiwe dira mpya za maji – Serikali

Bomba la maji safi
Spread the love

SERIKALI imeagiza wananchi kuendelea kufungiwa dira mpya za maji – Lipa Kadiri Utumiavyo – ili kupunguza malalamiko yao. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hatua hiyo pia imeelezwa kuwa, itapunguza tatizo la malimbikizo ya madeni ya matumizi ya maji.

Jumaa Aweso, Naibu Waziri wa Maji ametoa kauli hiyo leo bungeni tarehe 2 Aprili 2019 bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Dk. Jasmine Bunga.

Katika swali lake, mbunge huyo alisema, kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi dhidi ya mamlaka za maji katika halmashauri kwa kuwapatia wananchi bili kubwa za maji ambazo haziendani na uhalisia.

“Je, ni lini serikali itaanzisha utaratibu wa kulipa maji kadri utumiavyo, katika utoaji wa huduma za maji kama ilivyo kwenye umeme,”amehoji.

Aweso akijibu swali hilo amesema, serikali imeishaanza kutumia utaratibu wa kulipa maji kadri unavyotumia katika maeneo mbalimbali nchini.

“Kwa sasa utaratibu huo umeanza kutumika katika maeneo yanayohudumiwa na Mamlaka za Arusha, Iringa, Songea, Dodoma, Tanga, Mbeya, Tabora, Mwanza, Moshi na DAWASA,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!