Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanakijiji waamua kujenga sekondari, wamuangukia Rais Samia
Elimu

Wanakijiji waamua kujenga sekondari, wamuangukia Rais Samia

Spread the love

 

WANANCHI wa Kijiji cha Wanyere, Wilaya ya Musoma Vijijini mkoani Mara, wamemua kuanza ujenzi wa shule ya sekondari kwa ajili ya kuwaondolea wanafunzi adha ya umbali mrefu kufuata elimu katika vijiji jirani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Wakizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni wakati wakiandaa eneo la ujenzi wa sekondari hiyo, wanakijiji hao wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, pamoja na Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, kuwaunga mkono katika ujenzi huo.

Judith Chibunu, mkazi wa Kijiji cha Wanyere, amesema wananchi wamemua kujenga shule hiyo baada ya watoto wao kukabiliwa na changamoto ya kutembea umbali mrefu kwenda vijiji vya jirani ambako Kuna shule.

“Tumeamua kufungua shule hii ili watoto Wetu wapate elimu bila changamoto, kwa Sasa wanalazimika kuvuka vijiji vitatu kufuata shule. Serikali ya Rais Samia ni sikivu tunaomba ituunge mkono ili shule hii ikamilike,” amesema Chibunu.

Kwa upande wake Kaimu Mtendaji wa Serikali ya Kijiji cha Wanyere, Hanifa Ibrahim, amesema mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa shule hiyo ni mkubwa, hali inayoonyesha kwamba Wana dhamira ya dhati ya kuhakikisha watoto wao wanapata elimu Bora.

Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Muhongo ameunga mkono juhudi za wananchi hao kwa kuchangia mifuko 100 ya saruji.

Taarifa ya ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, imesema lengo la ujenzi wa shule hizo kwa kutumia nguvu za wananchi ni kuhakikisha zinafunguliwa na kuanza kutoa huduma kuanzia Januari 2024.

Kijiji cha Wanyere kinafuata nyayo za vijiji vingine 67 vya Jimbo Hilo kujenga shule za sekondari kwa nguvu zao pamoja na misaada kutoka kwa wadau wa maendeleo, ili kutatua changamoto ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata shule zilizoko katika vijiji vya jirani, pamoja na mrundikano wa wanafunzi.

Ofisi ya Prof. Muhongo imetoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kutoa michango Yao ili kufanikisha ujenzi wa shule hizo pamoja na maabara za masomo ya sayansi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!