Wednesday , 29 March 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Wanafunzi St Marys wazichachafya shule 59, Ni katika Quiz iliyoandaliwa na TRA
Elimu

Wanafunzi St Marys wazichachafya shule 59, Ni katika Quiz iliyoandaliwa na TRA

Spread the love
WANAFUNZI wa shule ya St Mary’s Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, wameibuka kidedea kwenye shindano la kujibu maswali mbalimbali yanayohusu kodi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Shule hiyo iliibuka nafasi ya pili ikitanguliwa na shule ya sekondari ya Kibaha mkoani Pwani katika shindano hilo lililofanyika kwenye Chuo cha Kodi Mikocheni.

Shindano hilo lililodumu kwa siku tatu liliendeshwa hivi karibuni na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kushirikisha shule 59 za sekondari binafsi na za umma.

Akizungumzia shindano hilo jana, Mwenyekiti wa bodi ya shule hizo, Dallas Mhoja alisema kufuatia ushindi huo wanafunzi wa shule hiyo walizawadiwa kompyuta, mashine ya kudurufu, kombe na medali mbalimbali.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), akimpa zawadi ya ngazo mwanafunzi wa kidato cha nne wa shule ya St Mary’s High School, Sia John baada ya wanafunzi wa shule hiyo kushika nafasi ya pili kati ya shule 59 katika mashindano ya kujibu maswali kuhusu kodi yaliyofanyika hivi karibuni8

“Huwa tunashiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa na TRA kwa hiyo mwaka huu tumeshiriki zilikuwa shule 59 na katika hizo shule tulibuka washindi wa pili nyuma ya Kibaha iliyokuwa ya kwanza,” alisema

Aidha, alisema tukio hilo limefanywa na taasisi kubwa ya serikali kwa kushirikisha shule binafsi na za serikali hivyo ushindi wa shule hiyo ni jambo la kujivunia kwa uongozi mzima wa shule.

Alisema wanafunzi wa shule hiyo walionyesha umahiri wa hali ya juu katika kujibu maswali mbalimbali yanayohusiana na kodi hali iliyowafanya kuibuka wa pili.

Wajumbe wa bodi na walimu wa shule ya St Mary’s High School wakiwa kwenye picha na zawadi walizopewa na TRA kwa shule hiyo kuwa ya pili kati ya shule 59 kwenye shindano la Quiz kuhusu masuala mbalimbali ya kodi iliyofanyika hivi karibuni kwenye chuo cha kodi Mikocheni

“Kushindana na shule 59 za Mkoa wa Dar es Salaam, zikiwemo za binafsi na za serikali na kuibuka kwenye nafasi ya pili tunaona siyo jambo dogo kwetu. Tunajivunia mafanikio haya na mashindano yajayo tutashika namba moja,” alisema

Alitaja siri ya mafanikio hayo kuwa ni maandalizi mazuri ya wanafunzi na walimu wenye kuipenda kazi yao ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana.

“Shindano hili limeleta msisimo mkubwa sana kwa wanafunzi wetu na walimu walioshiriki kwasababu mbali na zawadi kama kompyuta walizawadiwa fedha taslim kwa hiyo mashindano haya ni muhimu sana,” alisema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

Elimu

Mfuko wa Jimbo Musoma Vijijini wamwaga mamilioni ujenzi maabara za sekondari

Spread the love  MFUKO wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mkoa wa Mara,...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Elimu

Harambee ujenzi sekondari za Musoma Vijijini yashika kasi

Spread the love  HARAMBEE ya ujenzi na ukarabati wa shule za sekondari...

error: Content is protected !!