MAMIA ya wananchi wanaendelea kujitokeza katika uzinduzi wa kampeni za urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zinazofanyika leo Ijumaa tarehe 28 Agosti 2020, Uwanja wa Zakhiem, Mbagala jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Tundu Lissu ndiye anayepeperusha bendera ya Chadema kwenye nafasi ya urais na Salumu Mwalimu mgombea mwenza.
Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema bara na Mwalimu, naibu Katibu Mkuu-Zanzibar tayari wamewasili uwanja hapo.
Soma zaidi:-
Ulinzi umeimarishwa katika viwanja hivyo, ambapo kuna baadhi ya askari polisi wa kawaida na wale wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU).
Pia, kuna walinzi maalum wa Chadema ambao wanafanya kazi ya kuongoza watu waliofika katika kampeni hizo.
Kampeni za Uchaguzi Mkuu zilifunguliwa rasmi tarehe 26 Agosti na zitahitimishwa tarehe 27 Oktoba 2020 ambapo kesho yake yaani Jumatano itakuwa ni siku ya uchaguzi.
Katika uchauzi huo, Lissu atachuana na wagombea wengine 14 akiwemo Dk. John Magufuli, mgombea wa Chama cha Cha Mapinduzi (CCM), Prof. Ibrahim Lipumba (CUF), Yeremia Maganja (NCCR-Mageuzi).
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV ambao tuko live Youtube na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali
Leave a comment