Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Wambura hatunaye tena katika soka
Michezo

Wambura hatunaye tena katika soka

Michael Wambura
Spread the love

KAMATI ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imemfungia maisha kutojiusisha na soka Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho hilo, Michael Wambura baada ya kukutwa na hatia katika mashitaka matatu yaliyokuwa yakimkabili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Wambura amekupewa adhabu hiyo baada ya kukutwa na hatia ya kupokea fedha zisizo halali kiasi cha Sh. 84 milioni, pamoja na kukutwa na hatia ya kujipatia fedha, kwa njia ya udanganyifu na kughushi nyaraka sambamba na kula njama ya kulipwa fedha na waliokuwa viongozi wa TFF Jamari Malinzi na Celestine Mwesigwa ambao kwa sasa wanakabiliwa na kesi Mahakamani.

Kamati hiyo imetoa hukumu kwa Wambura kutojihusisha na soka kwa mujibu wa kifungu cha 73(1) (c) cha Kanuni za Maadili ya TFF Toleo la 2013. Baada ya kupatikana na makosa matatu, kamati hiyo ya maadili imefika maamuzi hayo kwenye kikao chao walichokutana jana (Jumatano).

Jana mchana afisa habari wa TFF Clifford Mario Ndimbo aliwaambia waandishi wa habari kwamba Wambura amefanya makosa hayo huku akijua anashusha hadhi ya shirikisho hilo ikiwa ni kinyume na katiba ya TFF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!