Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliotoroka Mgambo wapewa siku mbili kurudi kambini
Habari Mchanganyiko

Waliotoroka Mgambo wapewa siku mbili kurudi kambini

Spread the love

VIJANA takribani 200 waliotoroka katika mafunzo ya mgambo wapewa saa 48 ambayo ni sawa na siku mbili kurudi kambini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa mapema leo tarehe 1 Oktoba 2018 na Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Mhandisi Zephania Chaula wakati akifungua mafunzo ya mgambo katika kijiji cha Terrat mkoani Arusha.

Pia, Mhandisi Chaula amewaagiza wenyeviti wa vijiji na vitongoji kwa kushirikiana na watendaji wa kata kusimamia utekelezwaji wa agizo hilo ili vijana hao warudi kwa ajili ya kuendelea na mafunzo.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Chaula amewataka vijana wanaoendelea na mafunzo ya mgambo kuzingatia mafundisho yao ili baadae wawe tegemeo kwa taifa katika shughuli za ulinzi na usalama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!