Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliotekeleza ghasia Cameroon wamtibua rais
Kimataifa

Waliotekeleza ghasia Cameroon wamtibua rais

Rais wa Cameroon, Paul Biya
Spread the love

RAIS wa Cameroon, Paul Biya amelaani ghasia zilizotekelezwa na wananchi na kusababisha mauaji ya watu nane wakati wa maandamano ya raia wa nchi hiyo, anaandika Catherine Kayombo.

Maandamano hayo yaliyofanywa  na wazungumzaji wa lugha ya kingereza nchini humo wanaotaka kujitenga na kupewa eneo lao, yaliingiliwa kati na polisi na kusababisha raia hao kupigwa risasi.

Ghasia hizi zimetokea wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini na sita tangu kujumuishwa kwa jimbo la wazungumzaji wa kiingereza ndani ya Cameroon.

Aidha rais Biya amewataka wananchi kutotenganishwa na itifaki za lugha kati yao, na kudai kuwa mgogoro wa lugha unaweza sababisha vita ya wao kwa wao.

Wazungumzaji wa lugha ya kingereza nchini Cameroon kwa uchache wao wamekuwa wakiandamana takribani mwaka sasa wakidai kubaguliwa hasa katika mfumo wa elimu na sheria ukilinganisha na wale wanaozungumza lugha ya Kifaransa.

 

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!