Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliotekeleza ghasia Cameroon wamtibua rais
Kimataifa

Waliotekeleza ghasia Cameroon wamtibua rais

Rais wa Cameroon, Paul Biya
Spread the love

RAIS wa Cameroon, Paul Biya amelaani ghasia zilizotekelezwa na wananchi na kusababisha mauaji ya watu nane wakati wa maandamano ya raia wa nchi hiyo, anaandika Catherine Kayombo.

Maandamano hayo yaliyofanywa  na wazungumzaji wa lugha ya kingereza nchini humo wanaotaka kujitenga na kupewa eneo lao, yaliingiliwa kati na polisi na kusababisha raia hao kupigwa risasi.

Ghasia hizi zimetokea wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini na sita tangu kujumuishwa kwa jimbo la wazungumzaji wa kiingereza ndani ya Cameroon.

Aidha rais Biya amewataka wananchi kutotenganishwa na itifaki za lugha kati yao, na kudai kuwa mgogoro wa lugha unaweza sababisha vita ya wao kwa wao.

Wazungumzaji wa lugha ya kingereza nchini Cameroon kwa uchache wao wamekuwa wakiandamana takribani mwaka sasa wakidai kubaguliwa hasa katika mfumo wa elimu na sheria ukilinganisha na wale wanaozungumza lugha ya Kifaransa.

 

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!