Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliotaka viongozi wafe kwa COVID-19 wakamatwa
Habari Mchanganyiko

Waliotaka viongozi wafe kwa COVID-19 wakamatwa

Spread the love

 

WATU wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kupendekeza majina ya viongozi wa serikali wanaotamani wafe kwa virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu tarehe 22 Februari 2021 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Nyigesa amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Frank Nyange (47), Moses Mgao (34), Mohamed Lutambi (47) na Bumija Senkondo (54).

Nje ya kutuhumiwa kupendekeza majina ya viongozi wanaotamani wafe kwa Covid-19, watuhumiwa hao wanadaiwa kutumia mitandao ya kijamii kusambaza taarifa za uongo juu ya vifo vya baadhi ya watu, waliodai wamekufa kwa Covid-19.

Kamanda Nyigesa amesema, Jeshi la Polisi linaendelea kuwasaka watuhumiwa wengine wanaodaiwa kusambaza taarifa za uongo juu ya Covid-19.

“Watuhumiwa hawa wanne tuliowakamata na wengine ambao tunaendelea kuwatafuta,  wanasambaza taarifa za uvumi juu ya vifo vya watu wanaodai wamekufa kwa Corona.

“Pia wanapendekeza majina ya viongozi wa serikali ambao walitamani wafe haraka kwa corona,” amesema Kamanda Nyigesa.

Kamanda huyo amewataka wananchi kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, kwa kusambaza taarifa za uvumi kuhusu vifo vya watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!