Saturday , 10 June 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Waliopata ujauzito kurudi shule
ElimuTangulizi

Waliopata ujauzito kurudi shule

Mwanafunzi mjamzito
Spread the love

 

SERIKALI imesema imeamua kuondoa vikwazo vya elimu hususani kwa wasichana ambao wamekatisha masomo yao kwa kukumbwa na matatizo mbalimbali ikiwamo kupata ujauzito. Anaripoti Danson Kaijage- Dodoma … (endelea).

Hayo yameelezwa na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu mafanikio na changamoto za wizara hiyo katika kipindi cha miaka 60 iliyopita.

Prof. Ndalichako amesema serikali imeamua kuondoa vikwazo vya elimu kwa watoto ambao wanakumbana na changamoto zilizokatiza masomo yao.

Amesema wapo baadhi ya watoto ambao wanashindwa kumaliza masomo na kukosa fursa ya kupata elimu jambo ambalo litaathiri maisha yao.

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako

“Tunajua wapo baadhi ya watoto ambao wamepata ujauzito, serikali imeamua kwamba wanapokuwa tayari… watarudi darasani na watafanya mitihani kama kawaida na wakifaulu watapangwa katika shule za serikali” amesema Prof. Ndalichako.

Neema hiyo pia inawaangukia hata vijana wa kiume ambao wamekatiza masomo yao hivyo watakapokuwa tayari ndani ya miaka miwili wataweza kuendelea na masomo yao na watakapokuwa wamefaulu watapangwa katika shule za serikali.

Sambamba na hilo Prof. Ndalichako amesema kuwa hata wale ambao walifutiwa matokeo ya mitihani wanayofursa ya kurudia mitihani kwa lengo la kutoikosa fursa hiyo muhimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!