Waliopatikana na hatia ya kumua Mawazo, ambaye alikuwa mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mkoa wa Geita, ni pamoja na aliyekuwa mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiy, Alfan Apolnar.
Wengine walioadhibiwa kunyongwa hadi kufa, ni mshitakiwa wa pili katika kesi hiyo, Epafra Zakaria, mshitakiwa wa tatu, Hashim Sharif na aliyekuwa mshitakiwa wa tano, Kalulinda Bwire.
Wote kwa pamoja walidaiwa kumuua kada huyo wa Chadema ambaye alikuwa pia mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Ziwa, tarehe 14 Novemba mwaka 2015.
Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa mahakamani, washitakiwa wote hao, pamoja na kukana madai hayo mahakamani, lakini walitajwa na mashahidi karibu wote wa Jamhuri kuhusika na mauaji hayo.
Mawazo aliuawa siku chache baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Katika uchaguzi huo Mawazo aligombea ubunge jimbo la Busanda.
Katika shauri hilo namba tisa la mwaka 2019, mshatakiwa wa nne, Habibu Feruzi ameachiwa huru baada ya ushahidi uliotolewa mahakamani hapo kushindwa kuthibitisha kuhusika kwake kwenye mauaji hayo ya kukusudia.
Hakimu mwandamizi mwenye mamlaka ya juu kusikiliza kesi ya mauaji, Frank Mahimbali, ameieleza mahakama kuwa baada ya kuitafakari kesi yote na kusikiliza upande wa mashtaka na mashahidi 13 pamoja na vielelezo vitano na ushahidi, mahakama imewakuta na hatia washtakiwa wanne.
Leave a comment