Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waliokufa kwa njaa Kenya wafikia watu 73, walifunga ili kukutana na Yesu
Kimataifa

Waliokufa kwa njaa Kenya wafikia watu 73, walifunga ili kukutana na Yesu

Spread the love

 

IDADI ya maiti zilizofukuliwa na polisi nchini Kenya zimefikia 73. Watu hao waliofunga hadi kufa walikuwa wafuasi wa Kanisa la Good News International jamii moja ya kikristo lililopo katika Kaunti ya Klilifi nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Maiti hizo zimefukuliwa kwenye makaburi ya jumuiya yaliyopo msituni wa Shakahola uliokuwa unamilikiwa na mchungaji wa kanisa hilo Paul Mackenzie.

Mkuu wa upelelezi wa kaunti ya Kilifi, mashariki ya Kenya, Charles Kamau amethibitisha idadi hiyo na ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba watu wengine watatu wamekamatwa.

Shirika la msalaba mwekundu la nchini Kenya limesema watu 112 hawajulikani walipo.

Rais William Ruto amesema kiongozi wa jamii hiyo ya kikristo ni mhalifu mkubwa.

Paul Mackenzie alikamatwa takriban wiki mbili zilizopita baada ya fununu juu ya kuwepo kwa makaburi yaliyokuwa na maiti 31 za wafuasi wake.

Wafuasi wa kanisa la Good News International walikuwa wanaishi kwa kujitenga kwenye eneo la ekari 800 za msitu wa Shakahola nchini Kenya.

Inatuhumiwa kwamba waliagizwa kufunga mpaka kufa ili kuweza kukutana na Yesu.
Idara ya upelelezi ya nchini Kenya imesema watu 33 wameshaokolewa hadi sasa.

1 Comment

  • VIONGOZI WANAOONGOZA KUKOSOA MAAMUZI YA VIONGOZI WENZAO TANZANIA….. KWA MBINU ZOTE TULIZANI HUWA MANAKUBALIANA
    Mwanasiasa maarufu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche ametema cheche kuhusu sakata linaloendelea la Kampuni ya Twiga Cement kutaka kuinunua Kampuni ya Tanga Cement.

    Her Excel. Samia Suluhu

    Mr. Daniel Chongolo

    Mr. Professor Ibrahim Haruna

    Mr. Hamad Masoud Hamad

    Mr. Freeman Aikael Mbowe

    Mr. John John Mnyika

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!