Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walioacha masomo zaidi ya 3,000 warejea shule
Elimu

Walioacha masomo zaidi ya 3,000 warejea shule

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema wanafunzi zaidi ya 3,000 walioacha masomo kwasababu mbalimbali, wamerejea masomoni baada ya Serikali yake kutoa muongozo wa namna ya kurudi shule. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo kupitia mahojiano yake na Kituo cha Televisheni cha Azam, yaliyorushwa leo Jumatano, tarehe 4 Mei 2022.

Mkuu huyo wa nchi, amesema wanafunzi 909 wa kike na wa kiume, walioacha masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo kupata ujauzito wakiwa shuleni, wamerejea masomoni katika shule za kawaida, huku 3,000 wakijunga na vyuo vya ufundi stadi ikiwemo VETA.

Rais Samia amesema, Serikali yake imetoa muongozo huo ili kufuta doa lililowekwa kwa Tanzania na ulimwengu , ya kwamba inanyima haki ya wanafunzi hao kurudi shule hususan wasichana wanaokutana na changamoto ya kupata ujauzito wakiwa shule.

“Nilipokuja tukalikataa suala hili, nikaona kwa nini tugombane na ulimwengu tujitie doa. Na uzuri mimi nilisema wanafunzi wote, sababu kuna wavulana waliacha shule wako wanajutia walichokifanya nilisema wote walioacha shule warudi,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia amesema wadau mbalimbali wanaendelea na zoezi la uchukuaji maoni kuhusu marekebisho ya vipengele vya Sheria ya Ndoa, vinavyohamasisha ndoa za utotoni.

“Maoni ya wadau yanaendelea kuchukuliwa, waangalie kwa vizuri waone njia sababu jambo hili linaangaliwa zaidi na viongozi wa taasisi za dini, kuna dini zinasema mtoto akishabalehe kama anaweza kuolewa aolewe, sasa ukitoa kauli wanaweza sema hawa wanavunja dini yetu,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!