Saturday , 30 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Walinzi wa amani UN waondoka Mali
Kimataifa

Walinzi wa amani UN waondoka Mali

Spread the love

MALI imeendelea kuwa na usalama hafifu hali iliyolazimu Ujumbe wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa (MINUSMA) nchini humo, kuondoka leo Jumatatu kutokana na mashambulizi yanayohatarisha ulinzi wao. Anaripoti Mlelwa Kiwale, TUDARCo, kwa msaada wa Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Hatua hiyo imejiri baada ya jeshi la Mali (FaMa) kusema takribani wanajeshi wao wanane wamejeruhiwa na wengine saba wameuawa katika mashambulizi yaliyoyafanywa na waasi wa zamani kupitia uongozi wa kikundi cha waasi cha Azawad (CMA).

Pia wanajeshi wa nchi hiyo waliwaua waasi takribani 28 na kuweka ulinzi katika mji wa Ber ambapo uliokaliwa na kikosi hicho cha kulinda amani nchini humo.

Kikosi hicho kilisema msafara wao ulishambuliwa mara mbili na watu wao watatu kujeruhiwa na kupelekwa hospitalini Timbuktu kwa matibabu zaidi.

Hivyo, mashambulizi hayo yaliwawalazimu wao kuondoka mapema katika mji wa Ber kaskazini mwa mali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!