Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu tuache kufundisha kwa mazoea: Rais Samia
Elimu

Walimu tuache kufundisha kwa mazoea: Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa walimu wote nchini kuacha kufundisha kwa mazoea na badala yake wajifunze mbinu mpya za kufundisha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Mkuu huyo wa nchi ametoa wito huo leo Jumanne tarehe 10 Januari, 2023 wakati wa ufunguzi wa skuli ya Msingi ya Mwanakwerekwe ikiwa ni maadhimisho ya miaka 59 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mbali na walimu pia Rais Samia amesisitiza haja ya kufanya mabadiliko ya mitaala ya elimu ili wanafunzi waweze kuchukua masomo machache yatakayowasaidia kuwa na ujuzi wa kutosha kuliko kuchukua masomo mengi ambayo mwishoni humchanganya.

“Jack of all master of none,” Rais Samia ametumia nahau hiyo ya Kiingereza kuonesha namna mwanafunzi anayebeba masomo mengi asivyoweza kumudu somo lolote.

Pia Rais Samia ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwa makini na matumizi ya simu ya watoto wao na kuhakikisha kuwa wanazitumia katika kujifunza zaidi kuliko masuala ya burudani.

Shule hiyo ambayo imepewa jina la Dk. Samia itakuwa na uwezo wa kuchukua wananfunzi 1,300 na imejengwa kwa Sh 4 bilioni ikiwa ni matumizi ya fedha za nafuu ya Uviko-19.

Rais Samia amejitolea kuwa mlezi wa shule hiyo pamoja na iliyopo jirani na hiyo ya Dk. Magufuli ambapo amesema itafunguliwa akaunti maalum na kwa kuanzia ameweka Sh 20 milioni kwaajili ya kuhudumia shule hizo mbili.

Amesisitiza walimu kuhakikisha uzuri wa jengo hilo la ghorofa, unaendana na kile kitakachozalishwa hapo kwa maana ya matokeo mazuri ya wanafunzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!