Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Walimu Pemba wapigwa marufuku kwenda harusini
Habari Mchanganyiko

Walimu Pemba wapigwa marufuku kwenda harusini

Baadhi ya Walimu wa shule za sekondari na msingi mkoani Pemba
Spread the love

WALIMU wa Shule za msingi na sekondari katika mkoa wa Kaskazini Pemba visiwani Zanzibar wamepigwa marufuku kwenda katika sherehe hasa harusi wakati wa kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman, kwa kusema kuwa serikali haitamvumulia mwalimu atakayetoroka shule kwenda harusini, na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria.

RC Othman amesema kuwa, baadhi ya walimu wamekuwa na desturi ya kwenda harusini wakati wa muda wa kazi hasa siku za ijumaa, ambapo amekemea tabia hiyo kwa kuwa ni kinyume na sheria za utumishi wa umma.

Aidha, amewataka wakuu wa shule mkoani humo kutotoa ruhusa kwa walimu wenye tabia za kuondoka shule wakati wa kazi kwa ajili ya kwenda katika sherehe mbalimbali, na kuagiza walimu hao kama wanataka kwenda shughulini kusubiri muda wa kazi utakapoisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!